Monday, 24 January 2011

naomba nizungumze kitu.

Ndugu zangu nakuja kwenu leo kuzungumza nanyi  ili kila mmoja wenu anielewe, najua kila mmoja anajua vile ambavyo sifurahii maisha haya ambayo ninayo.
tatizo nililonalo mwenzenu sijui namna ambayo naweza kutoka katika tatizo hili
 nimejaribu kufikiria  kadri niwezavyo lakini akili yangu inagoma.

 kati ya  jamaa zangu  ama ndugu zangu  wengi  wamepiga hatua kutoka   moja kwenda nyingine kwa msaada wa mawazo yangu .
 jamani ndugu , jamaa na marafiki naomba mnisaidie ili niweze kutoka katika dimbwi hili la matope ambalo kimsingi naona nimeshafika  shinngoni bado kidogo sana kabla ya kuzama na kupotea kabisa.
hofu yangu ni kwamba kichwa changu ni kati ya vichwa vichache sana lakini kinaweza kisitumike kabisa kutokana na  ukosefu wa imani juu yangu .
 sijui ni kwa nini watu hawana imani na mimi?
 hata hivyo si wote ni braza wangu mkubwa  ambae haniamini kwa chochote .
 kwa kweli depretion  zote   ndani ya moyo wangu zinakuja  kwa ajili yake  kwani nimekua  na tatizo kubwa akilini  mwangu    ambalo ni kutafuta  kukubalika mbele yake  kitu ambacho sidhani kama kitakuja kutokea,
 ni sawa na kukimbiza kimvuli chako ukifikiria kwamba ipo siku utakikamata.
inaniuma sana.  

No comments:

Post a Comment